ONLINE

Saturday 26 November 2016

Bingwa wa riadha CASTER SEMENYA afanya harusi ya USHOGA! (PICHA)


Mbwembwe na furaha zilitanda katika kijiji kimoja cha Limpopo, Afrika Kusini, wakati wa sherehe ya kitamaduni ya ndoa ya mwanariadha Caster Semenya anayegubikwa na utata kuhusu jinsia yake.

Bingwa wa riadha CASTER SEMENYA afanya harusi ya USHOGA! (PICHA)
Caster Semenya (kulia) na mchumba wake.
Caster Semenya aligonga vichwa vya habari 2009 aliposhinda dhahabu katika mbio za mita 800 mjini Berlin, Ujerumani. Tangu wakati huo mwanadada huyo amegubikwa na utata kuhusu jinsia yake halisi. 

Semenya alilazimika kufanyiwa uchunguzi wa matibabu baada ya ripoti kuibuka kuwa alikuwa na homoni zaidi za kiume kuliko za kike.

Bingwa wa riadha CASTER SEMENYA afanya harusi ya USHOGA! (PICHA)
Semenya wakati wa harusi yao nyumbani Afrika Kusini.
Picha za kupendeza za mwanariadha huyo na mpenzi wake wa muda mrefu Violet Roseboya katika harusi ya kufana.

Cha kushangaza ni kuwa wanakijiji walichangamkia harusi hiyo ya jinsia moja katika bara la Afrika ambalo ni mwiko kuwa na ndoa za ushoga.

Bingwa wa riadha CASTER SEMENYA afanya harusi ya USHOGA! (PICHA)
Bingwa huyo wa mita 800 amegubikwa na utata kuhisi jinsia yake.
Katika sherehe hiyo, Semenya amevalia mavazi ya kitamaduni ya kiume huku mpenzi wake wa kike akiwa na mavazi ya kike.

Bingwa wa riadha CASTER SEMENYA afanya harusi ya USHOGA! (PICHA)
Ushoga bado ni mwiko katika mataifa chungu nzima ya Afrika.
Hata hivyo, licha ya ushahidi wa picha, Semenya amenukuliwa akikana kuandaa harusi ya kitamaduni ambapo alilipa KSh250,000 kama mahari kwa wakwe zake.

No comments:

Post a Comment